Jumatatu, 2 Juni 2014

NINI MAANA YA MAJIPU, DALILI ZAKE NA AINA YA MAJIPU PIA.

Majipu mara nyingi husababishwa na maambukizi ya bakteria, kawaida staph (Staphylococcus aureus). Hadi asilimia 80 ya watu kuwa na bakteria staph juu ya ngozi zao au katika pua wakati fulani katika maisha yao. Wengi wa wakati hakuna dalili ya majipu. Hii inaitwa ukoloni. Kuhusu 1 asilimia ya watu kuwa na aina maalum ya staph aureus aitwaye methicillin sugu staph (au MRSA kwa muda mfupi), ambayo ni sugu kwa baadhi ya antibiotics matibabu majipu na inaweza kuwa vigumu kutibu.

Aina ya majipu

Kuhusu aina mbalimbali ya majipu mtu anaweza kutofautisha zifuatazo ndio:
  • Furuncle au baharamani Aina hii ya majipu ni jipu ngozi kwamba alionekana kutokana na Staphylococcus aureus bakteria. Fursa ya furuncle juu ya ngozi inaweza kuwa na uhusiano na baridi. Zumaridi mara kwa mara ni seti ya follicles nywele ambayo fomu ni absess. Wakati mtu majipu sugu, yeye anaugua carbunculosis au furunculosis.
  • Acne cystic: Aina hii ya majipu hutokea baada ya clogging na maambukizi ya ducts mafuta. Acne cystic ina athari katika ngozi kushangaza tishu zaidi kwa kulinganisha na mara kwa mara acne , ambayo huathiri ngozi ya juu juu ngazi zaidi. Aina hii ya acne hutokea kwenye uso. Ujumla vijana wanakabiliwa na yake.
  • Hidradenitis suppurativa: Wakati abscesses wengi wamekusanyika katika maeneo ya kinena, na chini ya armpits, hii inaitwa Hidradenitis suppurativa. Hali hii ni maendeleo katika maeneo ambapo tezi jasho ziko. Wao ni na inflamed na kusababisha hali hii. Safu ya matibabu pamoja na si antibiotics tu, bali pia utaratibu wa upasuaji, ambao unaweka mbali ya jasho tezi wanaohusika na kuzuia kuvimba zaidi.
  • cyst Pilonidal: aina hii ya majipu iko katika Groove kati ya makalio. Pilonidal jipu mara nyingi huanza kama maeneo ya kuambukizwa ndogo ambayo ni alikasirishwa na shinikizo kupindukia na ni inflamed sababu ya hiyo. Basi eneo anapata kubwa na anarudi katika nodule imara, kuuma kwamba si vizuri kukaa. Wakati na kukaa kwa muda mrefu wakati wa safari baadhi, kwa mfano, nafasi hii na shinikizo tokoni ya sababu ya kuambukizwa.

Dalili za majipu

Dalili za majipu ni rahisi, ni kuchemsha kama utawala hutokea kwa ghafla kama bonge la rangi nyekundu ambayo husababisha maumivu katika 1-2 cm kufikia kipenyo. Ngozi karibu yake pia inaweza nyekundu au kuvimba. 

pus Kisha ni kusanyiko katika mapema ya. Polepole humkunjulia na inaweza kufikia ukubwa wa mpira wa gofu. Hukua kubwa na anapata chungu zaidi, wakati mwingine kufikia golf ball kawaida. Basi inakuwa ya rangi ya njano-nyeupe, ambayo bursts mwisho na machafu. Kawaida inachukua wiki mbili kwa ajili ya jipu kutoweka au hadi mwezi mmoja katika kesi nadra. Wakati majipu ni kidogo, hawana kuondoka makovu juu ya ngozi. Lakini kubwa majipu wanaweza kuondoka nao. 

Eneo la majipu wanaweza kuwa katika sehemu yoyote ya mwili, lakini eneo zaidi ya mara kwa mara ni juu ya uso, kwapani, shingoni matako, na mapaja - maeneo na follicles nywele ambayo wanakabiliwa na jasho au kutokana na msuguano. 

Majipu kuangalia kama matuta ambayo ni inflamed na kuleta maumivu . Majipu ni zilionyesha na acne cystic. Kama sisi kulinganisha na cysts Acne, majipu ni redder, kuvimba ni kubwa na huleta maumivu zaidi. 

zumaridi A mara kwa mara inaonekana juu ya mabega mapaja, na nyuma ya shingo kama kundi la majipu. Unaathiri ngozi kuwaambukiza zaidi juu ya kiwango cha kushangaza zaidi kuliko majipu tofauti kufanya. Ya mienendo ya maendeleo ya carbuncles ni polepole, ni vigumu kuponya na kuacha kovu juu ya ngozi. Saa carbuncles mara ni kushikamana na hali ya uchovu na homa. 


Maeneo ambayo majipu kiujumla kuonekana ni usoni, shingoni, kwapani, matakoni, sehemu za siri na mapajani. 

WASILIANA NASI KWA +255762285404 AU +255713354389 KWA MAELEZO ZAIDI NA TIBA.

Jumatatu, 7 Aprili 2014

Njia 5 za kupunguza tumbo kirahisi

WADADA au WAMAWAKE wengi wanatamani kuwa na matumbo madogo, lakini wengi hushindwa kufikia ndoto hiyo kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za uzazi na kupenda chakula. Makala hii inaangalia njia rahisi ya kupunguza tumbo. 

1. Uangalifu katika kula 
Epuka chakula chenye wanga, mafuta mengi na sukari. Badala yake unaweza kula matunda na mboga za majani. Vile vile samaki wa baharini si wabaya kwani hawana mafuta mengi. 

2. Namna ya kula 
Usiache kula kwani jambo hilo litakunyima nguvu, unatakiwa kula milo mitatu mpaka minne lakini kwa kiasi kidogo. Unatakiwa kukaa zaidi ya saa tatu kabla ya kula mlo mwingine. 

3. Mazoezi ya kawaida
Si lazima ufanye mazoezi makali kwa ajili ya kupunguza tumbo. Unaweza kufanya zoezi la kutembea badala ya kupanda basi, kama hufiki mbali sana. Kama unaweza kuogelea, unaweza kufanya hivyo mara kwa mara, hiyo pia itakusaidia. 

4. Zoezi maalum 
Kama unaweza kufanya zoezi la kulala chali na kukaa, 'abs exercise' unaweza kufanya kwa dakika chache kila siku. Hiyo itasaidia kukomaza misuli ya tumbo hivyo tumbo kutokulegea. 

5. Kunywa maji 
Maji yanasaidia mmeng'enyo wa chakula, hilo husaidia mtu kuwa na afya njema. Kwa kuwa mtu akiwa katika hatua za awali za kupunguza tumbo husikia njaa mara kwa mara, ni bora anywe maji badala ya kula.


WASILIANA NASI KWA +255762285404 AU +255713354389 KWA MAELEZO ZAIDI.

Osteoporosis:Mifupa milaini, myepesi na kusagika


Tatizo hili hujulikana kwa jina la kitaalamu kama Osteoporosis. Ugonjwa huu unatokana na kupunguka kwa protini na madini kwenye mifupa (madini chokaa/calcium). Hali hii hupelekea mifupa kuwa milaini na myepesi ambapo inaweza kuvunjika kirahisi. Kipindi cha utoto hadi kufikia umri wa miaka 30, ni kipindi ambacho mifupa hujijenga zaidi. Baada ya hapo mifupa huwa ina kawaida ya kupoteza madini zaidi.
Tatizo hili linatokea sana kwa watu wazima, hasa zaidi kwaa wanawake ambao wamefikia kipindi cha kukoma hedhi (menopause), kuanzia miaka 50. Ni kipindi ambacho wanawake hupungukiwa na homoni yenye kazi ya kuilinda na kuikinga mifupa. Tatizo hili huwapata wanawake zaidi kwa kuwa wana mifupa midogo na myembamba kuliko wanaume. Miaka mitano (5) hadi aba (7) tangu mwanamke kukoma hedhi hupungukiwa na madini chokaa kwa asilimia ishirini (20%), zaidi ya wanaume. Kuanzia miaka 65 hadi 70 wanawake na wanaume hupoteza madini chokaa kwaasilimia sambamba.
Nini cha kufanya
  1. Mazoezi hasa kipindi ambacho umriu mepiga hatua
  2. Kwa wale wenye uzito uliozidi, jitahidini kufanya utaratibu wa kupunguza
  3. Jitahidi kupata madini chokaa (calcium) kwa wingi (maziwa freshi, maziwa mgando, mboga za majani)
  4. Jitahidi kupata Vitamini D (mayai, maziwa, samaki, mboga za majani, pata jua)



   Virutubishi
Kwa ambao tatizo limekuwa kubwa, inawapasa kujitahidi kupata virutubishi ili kuirejeshea mifupa nguvu na uimara, pia kuondokana na maumivu.
Virutubishi vifuatavyo vimewasaidia wengi wenye tatizo hili.

WASILIANA NASI KWA +255762285404 AU +255713354389 KWA MAELEZO ZAIDI.




Aina ya ugonjwa na Suluhishi

SOMA KWA UMAKINI MKUBWA HAPA....

Ni vema tukafahamu ugonjwa unaosumbua mwanadamu, na vilevile tukatambua aina ya vyakula ambavyo tukila vitatusaidia kuondokana na tatizo.
Mwili wa mwanadamu ulivyoumbwa: Mwili wa mwanadamu umeumbwa ukiwa mkamilifua, usiokuwa na tatizo lolote. Siku mtu anapozaliwa, wengi wetu tunazaliwa tukiwa hatuna tatizo lolote.
Kawaida mwili wa mwanadamu umeumbwa  ukiwa mkamilifu kwa maana ya kwamba unatakiwa kujimudu wenyewe, pia kuwa na uwezo wa kujirejeshea afya ya mwili wake mwenyewe na kuweza kuishi maisha yasiyo na magonjwa.
Mwanadamu ameumbwa na anazaliwa na seli muhimu ndani ya mwili ambapo zina kazi kubwa ya kuhakikisha mwili upo sawa siku zote.
Seli hizi muhimu zinajulikana kwa jina la kitaalamu kama "adult stem cells"
Kadri tunavyokua hasa kuanzia miaka zaidi ya 25, uwezo wa mwili wa mwanadamu kuzalisha hizi seli hupungua. Hii husababishwa na stress (kimwili, kihisia, kimazingira) na lishe duni (vyakula na vinywaji vingi vimewekwa madawa kutoka mashambani hata viwandani). 

Utumiaji wa dawa za magonjwa kwa muda mrefu, utumiaji wa sigara na vinywaji vikali huchangia kwa kiasi kikubwa kuharibu na kuua hizi seli.
Umwagaji wa damu kwa njia ya ajali au aina yeyote ile husababisha upotevu wa seli mwilini.
Seli hizi hutambulika kama "masta seli”ndani ya mwili wa mwanadamu ambazo baadae hubadilika jina kutokana na sehemu ambapo zimesafiri na kuweka makao. Kwa mfano zikifika kwenye ini zinaitwa “Liver cells”, kwenye ubongo zinaitwa “Brain Cells, kwenye macho zinaitwa “Eye cells… n.k 
Bone Marrow:Seli hizi zinazalishwa na kiungo kijulikanacho kama bone marrow
Seli hizi kipingua kwenye kiungo cha ndani ya mwili husababisha kiungo hicho kutofanya kazi vizuri na kisha kiungo kupata tatizo. Mfano seli za kwenye kongosho zikifa au kupungua husababisha kongosho kutofanya kazi vizuri na hapo tatizo la sukari kwenye damu hutokea.
Kwa hiyo tukipata elimu ya vyakula itatusaidia kuwa makini na ulaji wetu ili tuishi mbali na magonjwa.

Jumamosi, 5 Aprili 2014

SHINIKIZO LA DAMU(HYPERTENSION)

Ni msukumo wa damu ulioko juu kuliko inavyotakiwa kwa muda mrefu. Msukumo wa damu huitajika mwilini ili kusambaza chakula,oksijeni na kutoa uchafu.
Uanishaji wa shinikizo la damu

Uanishaji
Systolic BP
Diastolic BP
Kawaida (normal)
<120
<80
Prehypertension
120-139
80-89
Kali (mild hypertension)
140-159
90-99
Kali kiasi (moderate hypertension)
160-179
100-109
Kali sana (severe Hypertension)
≥180
≥110
Shinikizo la damu husababishwa na nini?
Aina ya kwanza: Asilimia 90-95 sababu huwa hazijulikani na kitaalamu huitwa primary or essential hypertension. Ingawa vitu vifuatavyo vimehusishwa kupelekea kupata aina hii ya shinikizo la damu. Navyo ni:
  1. Uvutaji sigara
  2. Unene (visceral obesity)
  3. Unywaji wa pombe
  4. Upungufu wa madini ya potassium
  5. Upungufu wa vitamin D
  6. Kurithi
  7. Umri mkubwa
  8. Chumvi na madini ya sodium kwa ujumla
  9. Ongezeko la kemikali kwenye figo (renin)
  10. Kushindwa kufanyakazi kwa kichocheo kiitwacho insulin
Aina ya Pili: Asilimia 5 huwa na sababu dhahiri zinazopelekea kupata aina hii ya shinikizo la damu na huitwa kitaalamu secondary hypertension. Na sababu hizi ni:
  1. Hali ya kukosa hewa usingizini (sleep Apnea)
  2. Kasoro ya kuzaliwa nayo katika mshipa mkubwa wa damu (Coarctation of Aorta)
  3. Saratani za figo (wilm’s tumor, renal cell carcinoma)
  4. Saratani ya tezi iliyo juu ya figo (pheochromocytoma)
  5. Ujauzito – wapo wakina mama wajawazito ambao hupata shinikizo la damu na huwa hatarini kupata kifafa cha mimba (eclampsia)
  6. Magonjwa ya figo (renal artery stenosis, glomerulonephritis)
Dalili
Mara nyingi huwa hamna dalili zozote, na kama zikiwepo mgonjwa huwa na dalili zifuatazo:
  1. Uchovu
  2. Maumivu ya kichwa
  3. Kuhisi mapigo ya moyo kwenda haraka
  4. Kichefuchefu
  5. Kutapika
  6. Damu kutoka puani
  7. Kutoweza kuona vizuri (blurred vision)
  8. Kusikia kelele masikioni
  9. Na mara chache kuchanganyikiwa 
Madhara yanayoweza kuletwa na shinikizo la damu
  1. Kiharusi
  2. Moyo kushindwa kufanya kazi ( congestive heart failure)
  3. Madhara katika mshipa mkubwa wa damu ambapo ukuta wa ndani huchanika na damu hukusanyika katika ukuta wa mshipa huo(aortic dissection)
  4. Magonjwa ya mishipa ya damu
  5. Kushindwa kuona
  6. Athari katika ubongo 

KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI KWA +255762285404 AU +255713354389

Sigara huharibu DNA mwilini na kuongeza hatari ya kupata kensa!




Kemikali za sumu zilizoko katika tumbaku ya sigara huharibu DNA za mwili wa binadamu dakika chache tu baada ya mtu kuanza kuvuta sigara. Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa hivi karibuni, kemikali hizo zinazoitwa Polycylic Aromatic Hydrocarbons (PAHs) husababisha DNA ziharibike na kuongeza uwezekano wa mtu kupata kensa. Katika uchunguzi huo watalamu walichukua kemikali hizo katika miili ya wavuta sigara na kuzifanyia uchunguzi, ambapo waligundua kuwa, kemikali za PHA hubadilika haraka mwilini na kuwa sumu ambayo huharibu DNA baada ya kupita dakika 15 hadi 30 tangu kuingia tumbaku katika mwili wa binadamu. Sumu hiyo hubadilisha seli mwilini au kufanya mutation, kitendo ambacho huweza kusababisha kensa. Wataalamu hao wanasema, kitendo hicho hufanyika kwa haraka sana kama vile inavyoingizwa mada ya sumu kwenye damu kwa sindano. Habari hii ni tahadhari kwa watu wanaotaka kuanza kuvuta sigara, kwani takwimu zinatuonyesha kwamba, watu 3,000 hufariki dunia kila siku umwenguni kutokana na kensa ya mapafu, maradhi ambayo husababishwa kwa asilimia 90 na uvutaji sigara. Madhara ya kuvuta sigara kwa muda mrefu yanajulikana na wengi, ambayo ni pamoja na magonjwa ya moyo na kensa mbalimbali, lakini wataalamu wanatuasa ya kuwa, madhara ya sigara huanza pale tu mtu anapoanza kupiga pafu ya kwanza na kuingiza moshi wa sigara mwilini. Hivyo bado hujachelewa na unaweza kuacha sigara hii leo!

Tatizo la kukosa choo watoto wadogo au kuwa na choo kigumu.



Tatizo la kukosa choo watoto wadogo au kuwa na choo kigumu na jinsi ya kulitatua
Watoto wadogo hasa wale ambao bado wananyonya na ndio kwanza wamenzishwa vyakula vinginevyo zaidi ya maziwa, mara nyingi hupatwa na choo kigumu au kukosa choo kabisa hali tunayoiita kimombo, constipation. Hali hiyo huanza pale mtoto anapoachishwa maziwa ya mama na kuanza kunyweshwa maziwa ya kopo au mengineyo au pia anapoanzishwa kula vyakula vingine zaidi ya maziwa. Mara nyingi watoto wanaonyonya maziwa ya mama huwa hawasumbuliwa na tatizo hilo, bali tatizo hilo huanza kujitokeza pale wanapoanza kulishwa vyakula vingine zaidi ya maziwa ya mama. Pia mama ambaye tayari mwenyewe anasumbuliwa na tatizo la kukosa choo, huenda mwanae pia akasumbuliwa na tatizo hilo.
Mtoto mwenye tatizo la kukosa choo huwa anapata choo wa shida huku akisumbuliwa na tumbo na kupata choo kigumu. Wakati mwingine hulia wakati akipata choo huku akijiminya na kukunja uso. Muone daktari iwapo mtoto ana umri wa chini ya mwezi mmoja na hajapata choo kwa siku 4.